Tazama jinsi wengine wanavyofanya!

Soma kuhusu uzoefu wa watu wa Manobo katika kuweka kumbukumbu za Pangasananan hifadhi ya jadi katika Ufilipino, ikifanya kazi na wenyeji na washirika wa kimataifa na kutumia mbinu mbalimbali za ushirikishwaji na zana za kiufundi.

Kuweka kumbukumbu na kuwashirikisha jamii ya Pangasananan ya Watu wa Manobo wa Bislig (Mindanao, Ufilipino)

Imetayarishwa na Glaiza Tabanao, Ufilipino

Pangasananan ni jina la eneo la hifadhi ya jadi la watu wa Manobo, lililoko kaskazini-mashariki mwa kisiwa cha Mindanao, jiji la Bislig. Jina linatokana na neno la Manobo pangasan (yaani, kitendo cha kupata chakula na vifaa vya kukidhi mahitaji fulani, kama vile mbao, vifaa vitu vya ibada, mapambo, vifaa vya matumizi ya nyumbani, na kadhalika) na anan, kiambishi tamati kinachoashiria mahali. Mwanzoni ikiwa kubwa zaidi, Pangasananan ilikuwa eneo lililopakana na msitu mkubwa wa mbao kwa ajili ya mbao na karatasi, ambao umepunguza sehemu kubwa ya msitu wa awali. Sasa imebakia kilometa za mraba (km2) 70 tu, lakini inabaki kuwa chanzo cha kila kitu ambacho Manobo inahitaji—chakula, makazi, dawa, maji, burudani na sehemu za ibada, na kipato cha kujikimu kwa wanaume na wanawake wapatao 1,500. Kwa watu wa Manobo, kuharibu Pangasananan ingemaanisha anguko lao wenyewe, kufutika kwa utambulisho wao na kutowaheshimu kabisa mababu na mizimu yao. Kwa hiyo, ni muhimu kwao kutawala, kusimamia na kuhifadhi Pangasananan ili jamii yao istawi kwa vizazi vijavyo.

Wakati msukumo huu wa kuishi na kustawi ulipotishiwa na shughuli kubwa za ukataji magogo, uingiaji usiodhibitiwa wa wahamiaji, na upanuzi wa maeneo ya kilimo cha biashara katika eneo lao, vijana wa Manobo wa miaka ya mwanzo ya 1990 waliamua kupigana na kutafuta njia za kuzuia uharibifu na kupata kile kilichobaki cha Pangasananan yao.

Mapema katika mchakato huo, Manobo walitambua kuwa itakuwa vigumu kuendelea bila washirika. Kwa hiyo, walianzisha ushirikiano na kikundi cha kanisa la makazi yao, vikundi mbalimbali vyenye silaha, baadhi ya walowezi wahamiaji, na mashirika yasiyo ya kiserikali. Kampuni ya upasuaji mbao ilipowatisha kwa bunduki, kwa kawaida walitafuta bunduki kujilinda wao wenyewe na eneo lao. Kutoka kwa washirika wao wapya walikuwa wakitafuta ushauri, msaada wa kifedha na maarifa na ujuzi mpya waliohitaji kushinda hiyo vita. Walipata yote hayo. Kwa mfano, mnamo 2004 waliweza kuifahamu kanuni mpya iitwayo Kanuni ya Haki za Watu wa Kiasili, ambayo ingewaruhusu kupata Cheti cha Cheo cha Milki ya Kimila na kuhalalisha umiliki wa eneo lao. Hata hivyo, ili kupata hati hiyo, taarifa nyingi zinahitajika kukusanywa, kuthibitishwa, na kuwekwa pamoja kama uthibitisho wa umiliki wao wa eneo. Huu ukawa msukumo wa shughuli za kukusanya taarifa, uwekaji kumbukumbu na shughuli za ushirikishaji jamii.

.

.

Shughuli za uwekaji kumbukumbu zilikuwa nyingi na zilifuatiliwa haraka wakati mwaka 2009 jamii ilipofanya kazi na shirika lisilo la kiserikali lililoitwa Chama Cha Maendeleo ya Mila Ufilipino, Inc. Ingawa Chama Cha Maendeleo ya Mila Ufilipino, Manobo pia walifahamiana na Muungano wa Kongani la Kimataifa mwaka uliofuata. Wakati huo ndipo Manobo walitambua kwamba, wakati wakitaka kupata utawala wa eneo lao, walikuwa wanachangia pia kupambana na kuokoa mazingira ya asili. Waligundua kuwa walikuwa wakiishi, wakilala, wakilinda, kuhifadhi, na kupigania kile ambacho wengine wanakiita Kongani la Kimataifa au ‘eneo la hifadhi ya jadi’, lakini ambalo lilikuwa likijulikana kama Pangasananan yao. Kando na kuwa chanzo cha uwezeshaji, waliona ufahamu huo kama fursa ya kupata washirika zaidi katika kulinda eneo lao, kuboresha mipango ya uhifadhi, kukuza desturi za jadi, kukusanya maarifa na ujuzi zaidi, kuimarisha madai yao, na kuboresha hali zao za maisha. Kwa hivyo, jamii iliamua kuweka kumbukumbu ya Kongani la Kimataifa yao na kuiwasilisha ili ijumuishwe katika Masijala ya Kimataifa ya Kongani la Kimataifa. Mnamo 2017, madai yao ya kisheria juu ya Pangasananan yalitiwa nguvu kwa kujumuishwa katika mradi wa kitaifa wa Kongani la Kimataifa ambao ulitoa rasilimali kwa ajili ya kazi zao za uwekaji kumbukumbu. Mradi huo uliungwa mkono na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira Duniani na Serikali ya Ufilipino kupitia Ofisi ya Usimamizi wa Bioanuwai na Tume ya Kitaifa ya Watu wa Asili.


Taarifa gani zilikusanywa?

Kwa ombi lao la Cheti cha Cheo cha Milki ya Kimila, jamii iliweka kumbukumbu na kukusanya taarifa zifuatazo, kwa msaada kutoka kwa Chama Cha Maendeleo ya Mila Ufilipino:

  • ushahidi wa kihistoria wa eneo kukaliwa na matumizi ya eneo;

  • historia ya Manobo kama watu na kama jamii

  • mifumo ya maarifa na shughuli za asili, imani za kiroho, na mifumo ya utawala wa kimila;

  • picha za maeneo muhimu, alama muhimu, shughuli za kitamaduni na kipato cha kujikimu;

  • vinasaba vya ukoo na historia za ukoo;

  • simulizi na takwimu kuhusu maliasili;

  • mipango ya sasa ya jamii, hali, mahitaji, fursa, na matishio;

  • takwimu za kijamii kwa mapana na idadi ya watu;

  • maelezo ya kijiografia na hali ya eneo;

  • matumizi ya sasa ya ardhi na utengaji wa maeneo; na mipaka na ukubwa wa milki ya mababu ya Manobo.

Hapo awali ilifanywa ili kukidhi mahitaji ya serikali kwa utambuzi wa milki ya mababu zao na kuendeleza Mpango wa Maendeleo na Ulinzi Endelevu wa Milki, maelezo haya yalionekana kuwa muhimu kwa uwekaji wa kumbukumbu na usajili wa Kongani la Kimataifa yao na kufuatia uundaji wa Mpango wa Uhifadhi wa Jamii. Taarifa pia zilikusanywa kuhusu hifadhi yao ya hewa ukaa, shughuli za uhifadhi, maarifa ya jadi na matendo yanayochangia uhifadhi wa asili, matumizi ya ardhi yaliyosasishwa, maeneo yanayokumbwa majanga, na umuhimu wa kiikolojia na thamani ya bioanuwai ya Pangasananan.

 

Je, taarifa ilikusanywaje?

Taarifa zinazohitajika zilikusanywa kupitia utafiti shirikishi, kufahamu shughuli za kila siku za jamii, na mbinu za tathmini shirikishi ya haraka. Njia ya wazi na shirikishi ilitumika katika yote haya, ambapo iliruhusu uchambuzi wa kina wa taarifa, ilitoa fursa ya kujifunza kwa pamoja na uthibitisho mtambuka, na kukuzwa kwa hisia kali ya umiliki wa takwimu na taarifa miongoni mwa wanajamii. Hii ilihakikisha ubora, umuhimu na manufaa ya taarifa iliyokusanywa.

Hizi ndizo hatua tulizochukua:

1. Uamuzi huru na wa hiari

Kumbukumbu za Uamuzi huru na wa hiari zilizotolewa na Masijala ya kimataifa ya Kongani la Kimataifa zilitafsiriwa kwa lugha ya wenyeji na kujadiliwa na kundi la awali la viongozi na wanajamii. Kila sehemu ya kumbukumbu ilielezewa na kujadiliwa, pamoja na taarifa juu ya faida, faida na changamoto ya kupakia takwimu kwenye Masijala ya Kimataifa ya Kongani la Kimataifa na masuala ya umiliki wa takwimu, nk. Hatimaye, jamii iliamua kwamba manufaa ya kuelezewa kwa undani kwa eneo lao la hifadhi ya jadi yalikuwa muhimu zaidi kuliko vikwazo na hatari ambazo pia zilidokezwa.

2. Utambuzi na Mafunzo ya Wadau wa Utafiti wa Jamii

Wadau wa Utafiti wa Jamii walitambuliwa na wazee na viongozi wa jamii. Kisha walipewa maelekezo kuhusu malengo makuu na malengo ya utafiti pamoja na mbinu mbalimbali za utafiti na uzalishaji wa takwimu za eneo hilo la ardhi kwa kutumia mbinu za tathmini shirikishi. Hatimaye, walifunzwa jinsi ya kufanya tathmini shirikishi ya maliasili.

3. Utafiti Shirikishi

Utafiti shirikishi ulikamilika kupitia mbinu za msingi na za upili, ikijumuisha uchunguzi wa kuona kwa macho, mahojiano ya watoa taarifa muhimu, mijadala ya vikundi lengwa, na mapitio ya machapisho yaliyopo, kumbukumbu, na utafiti. Haya yalifanyika katika mazingira rasmi na yasiyo rasmi, njia yoyote ambayo ilifaa kutumika. Watoa taarifa walichaguliwa wakati wa mikutano na mahojiano ya viongozi na wazee. Timu ya watafiti pia ilitengeneza orodha hakiki zilizopo, kumbukumbu muhimu kutoka kwa jamii, intaneti, serikali na wasomi, na pia kutoka kwa kanzidata za mwanzo za Chama cha Maendeleo ya Mila Ufilipino.

Mada kuu za utafiti zilijumuisha historia ya Manobo; shughuli za jadi na za sasa za kipato cha kujikimu na ratiba mbalimbali; mifumo ya imani za kiroho; matambiko; usimamizi na matumizi ya maliasili; mifumo na miundo ya utawala wa jadi na wa kisasa; na historia, eneo, maelezo na hadithi kuhusu Pangasananan. Pia matishio kwa eneo la hifadhi ya jadi na watu wa Manobo kama wamiliki wake vilijadiliwa. Hatimaye, taarifa zilikusanywa kuhusu sanaa za jadi, ufundi, muziki, shughuli za uponyaji wa jadi; hadithi za kiroho; historia ya umuhimu wa maeneo ya kiutamaduni; mimea muhimu na matumizi yao; na matambiko (maelezo, nyenzo zilizotumika, na kwa nini zilitumika).

 

4. Ushirikishwaji jamii kutambua rasilimali za eneo lao

Utambuzi shirikishi wa rasilimali ulihusisha hatua kadhaa, zikiwemo:

  • Kubainisha taarifa muhimu za sura ya nchi kwa kutumia kifaa cha kuonesha mahali halisi Kijiografia;
  • Kutengeneza modeli ya ramani ya pande tatu (3-D);
  • Kuweka misimbo ya matumizi ya ardhi;
  • Kuweka takwimu za kidijitali na kuanzisha kanzidata ya Mfumo wa Taarifa za Kijiografia;
  • Uthibitishaji wa ramani ya eneo la jamii; na
  • Ukamilishaji wa ramani zilizoidhinishwa/ kanzidata ya Mfumo wa Taarifa za Kijiografia.

Wakisaidiwa na timu ya wataalam ya Chama Cha Maendeleo ya Mila Ufilipino, wanajamii waliofunzwa kutumia Mfumo wa Kuonesha Sehemu halisi za Kijiografia walifanya utafiti ili kubainisha eneo la Pangasananan. Walitembea kuweka alama za mipaka ya asili na alama za kitamaduni za milki. Pia walichukua alama muhimu za sura ya nchi ndani ya eneo. Hizi ni pamoja na eneo la majengo ya manispaa, shule, vituo vya afya, masoko, madaraja, barabara za zege na za vumbi, na mito na vijito. Takwimu zote zilizokusanywa ziliwekwa kwenye ramani ya eneo hilo. Kisha hii ilitumiwa kama ramani ya msingi ya kuazimu ukubwa wa eneo hilo.

Mnamo 2009, ramani ya pande tatu (3-D) yenye kipimo cha 1:10,000 ilikuwa tayari imetayarishwa na jamii kwa msaada wa Chama Cha Maendeleo ya Mila Ufilipino . Katika warsha za jamii, wataalamu wa Chama Cha Maendeleo ya Mila Ufilipino walikuwa wamewezesha shughuli za kuchora ramani ili kuwezesha jamii kutambua mipaka ya Pangasananan na kuamua ukubwa wake kamili. Washiriki wa jamii walikumbuka na kuandika majina ya milima, mito, maeneo matakatifu, na vijiji vya zamani katika lugha ya asili na kutoa maelezo ya kihistoria ya hizo rasilimali. Walitambua alama muhimu kama vile maeneo ya kuzikia, mapango, maziwa, mipaka ya maeneo ya jamii, misitu iliyohifadhiwa, na mengineyo. Hiyo michoro ya ramani ilikuwa msingi wa kuandaa ramani kubwa zaidi ya sura ya nchi na ramani za msingi ambazo zilitumika kuunda ramani ya muundo wa sura ya nchi katika eneo la kikoa chao: ramani ya 3-D!

Ramani ya 3-D iliyotengenezwa hasa kutokana na karatasi zinazopishana za mpira, resini na rangi ilitoa mwonekano kamili wa mambo ya asili mipaka ya eneo na sifa za kina za mwonekano wa milima na mabonde ya maji. Wazee walielezea matumizi ya sasa ya ardhi na kutambuliwa kupitia misumari midogo ya kugandamiza, nyuzi na kupaka rangi maeneo matakatifu, maeneo ya uwindaji, maeneo ya makazi ya zamani, n.k ndani ya ramani ya milki ya mababu. Kisha taarifa kutoka kwenye kikundi iliunganishwa na kuthibitishwa ili kuhakikisha kuwa ramani ilikuwa sahihi na inayofaa kwa mtumiaji.

Takwimu zilizotokana na ramani ya 3-D iliwekwa kidijitali kwa kutumia programu ya kompyuta (Toleo la Mfumo wa Taarifa za Kijiografia Quantum 2.14.0 na Mfumo wa Taarifa za Kijiografia  toleo la 10.1). Nakala za taarifa za kidijitali za uso wa ardhi kuhusu milki ya mababu/Kongani la Kimataifa/eneo la hifadhi ya jadi (tatu zilithibitishwa kuwa sawa kwa jamii) ziliwekwa kwenye kanzidata ya Mfumo wa Taarifa za Kijiografia na kutumika katika uzalishaji ramani kadhaa zenye mada tofauti. Utayarishaji na uchapaji wa ramani za mada mbalimbali ulikamilishwa na mtaalamu wa Mfumo wa Taarifa za Kijiografia wa Chama Cha Maendeleo ya Mila Ufilipino. Jumla ya ramani 23 zenye mada tofauti zilitolewa kutokana na utayarishaji shirikishi wa ramani na kupitia takwimu za Mfumo wa Taarifa za Kijiografia zilizopatikana kutoka serikalini, washirika wa taasisi zisizo za kiserikali, na majukwaa ya mtandao huria ya Mfumo wa Taarifa za Kijiografia kama vile Ramani za Google na Ramani ya OpenStreet. Ramani hizi zimeorodheshwa hapa chini:

  • Ramani ya Mahali
  • Ramani ya Mipaka ya Kongani la Kimataifa
  • Muingiliano wa Kongani la Kimataifa na maeneo mengine yenye Cheti cha Cheo cha Milki ya Kimila
  • Matumizi ya Sasa ya Ardhi/Jalada 2017
  • Jalada la zamani la Ardhi 1900
  • Jalada la zamani la Ardhi 1997
  • Jalada la zamani la Ardhi 2004
  • Mapendekezo ya Matumizi ya Ardhi
  • Upangaji wa Ardhi katika madaraja
  • Kambi/nyumba za wachimbaji madini
  • Mtandao wa Maeneo Yanayohifadhiwa kwa ajili ya Kilimo
  • Mtandao wa Maeneo Yanayohifadhiwa kwa Kilimo na Maendeleo ya Kilimo-Viwanda
  • Aina ya Udongo
  • Upangaji wa Mteremko katika madaraja
  • Muingiliano wa Kongani la Kimataifa na Mandhari inayohifadhiwa ya Tinuy-an
  • Muingiliano wa Kongani la Kimataifa na Bislig[1] Eneo Muhimu la Bioanuwai
  • Muingiliano wa Kongani la Kimataifa na Eneo Muhimu la Ndege la Bislig
  • Mipasuko ya ardhi
  • Maeneo yanayoweza kuathiriwa na Maporomoko ya ardhi
  • Maeneo yanayoweza kuathiriwa na Mafuriko
  • Mitandao ya Barabara
  • Mitandao ya Mito
  • Kuhesabu mali

Ramani sahihi na rahisi-kwa-mtumiaji ziliunganisha maarifa ya watu wa eneo hilo na takwimu za uso wa nchi kupitia teknolojia ya GIS kutumika kama chombo chenye nguvu cha mawasiliano na uchanganuzi bora. Ramani hizi zilikuwa muhimu katika kuelewa na kuelezea hali za mitaa, eneo la hatari, maeneo yanayohitaji upandaji miti na misitu inayohitaji ukarabati. Jamii pia ilitambua umuhimu wa eneo lao la jadi la – Kongani la  Kimataifa kama a chanzo cha maji kwa Bislig na kama chimbuko la viumbe hai. Jamii inaweza kutumia habari hii kuunda yao mapendekezo ya matumizi ya ardhi, shughuli na sera.

[1] Bislig ni mji huko Mindanao karibu na milki ya mababu cha Manobo na maarufu ya kuangalia nde

5. Tathmini Shirikishi ya maliasili

Tathmini Shirikishi ilifanyika ili kujua hali ya maliasili katika milki ya mababu. Orodha ya rasilimali ilitathmini hifadhi ya hewa ukaa kwenye miti na pia bioanuwai ya maua katika misitu ndani ya Pangasananan.

Njia ya utafiti ya kilomita 1, njia mbili za utafiti za mita 500 na viwanja viwili vya msitu wa hekta 0.25 vilianzishwa ndani ya Kongani la Kimataifa. Jumla ya hisa ya hewa ukaa iliyo juu ya ardhi ilitokana na milinganyo inayotumiwa na Wakfu wa Elimu Kalahan wakati bioanuwai ilikadiriwa kutumia wingi wa spishi na thamani za utofauti zinazotokana na Shannon pamoja na fahirisi za utofauti za Simpson.

Utafiti wa wanyama ulitegemea simulizi za zamani kutoka kwa wenyeji. Uorodheshaji huria wa majina na matumizi ya mimea na wanyama ambao walionekana na jamii pia ulifanyika. Picha za ndege na nyoka wanaojulikana zilionyeshwa kwa wanajamii ili kubaini ni aina zipi zilizoonekana mara kwa mara katika Pangasananan.

Taarifa pia zilikusanywa kuhusu aina ya mimea, eneo/makazi na huduma/thamani ambayo spishi-kiashirio za jadi (spishi za mimea zinazotambuliwa na jamii kama viashiria vya dalili ya afya ya msitu wao) hutoa kwa kabila na mazingira yake. Maana ya msitu na uwepo/kutokuwepo kwa spishi-kiashirio za kitamaduni kwa Manobo zilitumika kama msingi wa kutathmini afya ya misitu iliyoorodheshwa.

Uanzishwaji wa njia za kitafiti na tathmini ya bioanuwai kwa kutumia fahirisi zinazotumika kimataifa, pamoja na utambuzi wa spishi-kiashiria za jadi, zinaonyesha jinsi mbinu za kisayansi na jadi zinavyoweza kufaana katika mbinu rahisi ambazo jamii inazielewa, kuthamini na inaweza hatimaye kuzitumia ili kuimarisha utawala bora katika eneo lao la jadi.

 



Photos © Glaiza Tabanao