Kuweka kumbukumbu za eneo la hifadhi ya jadi: Maswali ya kujadili mashinani

Maswali haya yanaweza kusaidia jamii kuamua jinsi ya kutengeneza kumbukumbu za ziada kuhusu eneo lake la hifadhi.

  • Je, taarifa kuhusu eneo la hifadhi ya jadi zipo tayari na zinapatikana kwa urahisi kwa jamii yetu?
  • Je, imesambazwa kwa uwazi na kujadiliwa?
  • Ni miundombinu gani imetumika kuweka hiz taarifa muhimu – kwa mfano ramani, orodha, picha, hadithi, nyaraka…?
  • Je, kuna miundombinu ambayo inaweza kuwa muhimu hasa kwa jamii yetu? Kwa mfano, taarifa ya mdomo inapaswa kuwa kumbukumbu kupitia ushirikishwaji wa watu wote kwa kutumia ramani au filamu?
  • Je, kuna taarifa bado hazijapatikana/hazipo katika kumbukumbu na kwamba itakuwa muhimu kuwa nazo?
  • Je, hizi kumbukumbu zinawezakupatikanaje /kuundwa/kutengenezwa?
  • Je, jamii yetu itafanya nini na taarifa zilizopo katika kumbukumbu?
  • Kumbukumbu zitasambazwa vipi na nani? (Angalia pia #Chukua hatua na kufanya mawasiliano na #Chukua hatua ukiwa na wengine)
  • Je, kuna wasiwasi au hatari kutokana na kutengeneza au kusambaza kumbukumbuku? Je, tunawezaje kushughulikia hatari hizo?
  • Je, kuna fursa mpya kutokana na kutengeneza au kusambaza kumbukumbu? Je, tunawezaje kuchukua hatua juu ya haya?